Saturday 22 October 2016



OUT yamkumbuka Mwl Nyerere kwa Muhadhara 

Na Vincent Mpepo-OUT

Katika kuadhimisha miaka 17 ya kifo cha Baba wa Taifa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kimeadhimisha kwa kufanya muhadhara wa wazi ambao umeshirikisha wanazuoni katika fani mbalimbali chuoni hapo na mada kuu iliwasilishwa kama sehemu ya kukumbuka na kuenzi mchango wa muasisi huyo kwa  Taifa.

Akiwasilisha mada katika mhadhara huo, Mhadhiri Mwandamizi Dkt Neville Reuben alisema kuwa Mwl Nyerere alikuwa na maono ambayo kama yangeendelezwa kiutekelezaji yangesaidia kulifikisha taifa hili mbali katika nyanja zote za kisiasa, kiuchumi na kijamii kwani alisisitiza katika elimu.

“Mwl Nyerere aliamini kuwa elimu ndiyo nyenzo kuu ya kuondoa ujinga, umaskini na maradhi”, alisema Dkt. Reuben

Alisema kuwa Chuo kIkuu Huria cha Tanzania kipekee kitamkumkumbuka na kumuenzi muasisi huyo kwa juhudi na maono ya uanzishawaji wake kwani aliamini kuwa elimu haina mwisho na kwamba watanzania wengi wangeweza kupata elimu kupitia mfumo usio rasmi kupitia chuo hicho.

Alisema  elimu ndio msingi wa taifa lolote na kwamba kupitia Chuo Kikuu Huria cha Tanzania watanzania wanaweza kupata elimu ambayo itawasaidia kwenda sambamba na mahitaji katika soko la ajira kwa kusisitiza masuala ya kujiajiri katika sekta isiyo rasmi ikiwemo ujasiriamali wakati taifa likielekea kwenye uchumi wa kati.

Kwa upande wake, Dkt Lawi Yohana, ambaye alimuwakilisha Makamu Mkuu wa Chuo-Taaluma chuoni hapo alisema kuwa kuwa muhadhara huo ni sehemu ya elimu kwa jamii na utekelezaji wa majukumu ya chuo kikuu chochote amabayo ni ufundishaji, ushauri wa kitaalamu na kufanya tafiti.

Dkt Lawi alisema kuwa mhadhara huo ni mwanzo mzuri wa kuendelea kuenzi fikra za Mwl Nyerere huku tukijiuliza rasilimali tulizonazo na matumizi yake yanaendana vipi na falsafa za muasisi huyo.

Mkuu wa Idara ya Mawasiliano chuoni hapo, Bi Kahenga Dachi alisema kuwa lengo la mhadhara huo ni kuenzi yale yote ambayo Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyapigania kwa manufaa ya nchi  na bara la Afrika kwa ujumla.

Mhadhara huo umeratibiwa na Kurugenzi ya Masoko na Mawasiliano chuoni hapo na mada kuu ikiwa ni
“Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Chuo Kikuu Huria, Ujasiriamali na Uchumi wa Viwanda”.

Thursday 20 October 2016



Serikali kuhamasisha wananchi kuuelewa mpango wa kuondoa ukatili kwa wanawake na watoto
Na Vincent Mpepo-OUT
Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wa ndani na nje imekusudia kuanza utekelezaji wa mpango kazi wa miaka mitano wenye lengo la kumaliza kabisa vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto hapa nchini.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi Sihaba Nkinga wakati wa mafunzo ya siku moja kwa waandishi wa habari ikiwa ni maandalizi ya uzinduzi wa Mpango Kazi wa Kitaifa wa kumaliza ukatili kwa wanawake na watoto iliyofanyika jijini Dar es salaam.
Bi alisema kuwa serikali imekusudia kushirikisha waizara na idara mbalimbali katika utekelezaji wa mpango huo ili kujenga dhana ya upamoja na kuifikia Jamii kwa haraka hivyo kurahisisha upatikanaji wa taarifa muhimu kuhusu masuala ya haki za wanawake na watoto.
“Uhamasishaji kwa jamii kuuelewa mpango kazi huu ni jukumu la kila mmoja wetu hivyo tunapaswa kushirirkiana ili kufanikisha adhma hii ya kuwakomboa Wanawake na watoto dhidi ya vitendo vya ukatili dhidi yao”, alisema Bi Nkinga
Alisema kuwa serikali imejidhatiti kushirikiana na wadau wa maendeleo kufanikisha mpango huo ili kulinda hadhi tulipewa kama nchi kwa kuwa Tanzania ndiyo nchi pekee kwa Afrika amabayo imeonesha utekelezaji kwa vitendo ijapokuwa juhudi zaidi zinahitajika ili kufikia malengo.
Aidha alisema kuwa uhamasishaji na utekelezaji wa mpango kazi huo utahusisha asasi za kiraia na taasisi mabalimbali sizizo za kiserikali na dini.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto, Wizara ya  Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi Maragareth Mussai alisema kuwa mpango kazi huo umezingatia masuala mtambuka ikiwemo utengaji wa bajeti kwa makundi mbalimbali yanayojishughulisha na Wanawake na watoto.
“Bajeti imewekwa katika ngazi zote ili kurahisisha utekelezaji wa mpango kazi huu ikiwemo uwezeshaji kwa wafanyakazi katika idara mbalimbali katika ununuzi wa vifaa, vyombo vya usafiri na vitendea kazi”, alisema Bi Mussai.
Naye pedro Guerra, Mtaalamu wa Masuala ya Haki za watoto alisema kuwa watoto ni waathirika wakubwa wa vitendo vya ukatili hivyo huathirika kisaikolojia na makuzi ya ubongo wao.
“Matokeo ya tafiti tulizofanya yananoessha watato wa Tanzania wanakabiliwa na msongo wa mawazo katika ngazi ya familia, mazingira ya shule na wanaowafanyia ukatili huo ni ndugu wa karibu”, alisema Guerra. 
Madhumuni ya mafunzo hayo ya siku moja yalikuwa ni kuwafundisha waandishi wa habari namna ya kuripoti habari mbalimbalimbali kuhusu vitendo vya ukatili dhidi ya watoto na Wanawake Tanzania.

Saturday 27 August 2016

Ligalawisi:

Serikali Kushirikisha Wataalamu Kuikwamua Sekta ya Utalii, Ukarimu
Na Vincent Mpepo-OUT
Serikali imesema kuwa itaendelea kushirikisha wataalamu na watafiti katika kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazoikabili sekta ya Utalii na Ukarimu ili kuibua fursa na bidhaa mpya kupitia sekta hiyo kwa lengo la kuongeza pato la taifa.
Kauli hiyo imetolewa na Meja Jenerali Gaugence Milanzi, Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii wakati akifunga wa Kongamano la Kimataifa la Utalii, Ukarimu na Ubunifu  kwa Nchi zinazoendelea jijini Dar es salaam lililoandaliwa na Idara ya Utalii na Ukarimu ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Alisema kuwa kongamano hilo limekuwa mwanzo mzuri wa kuwakutanisha wataalamu, watafiti na wadau wa ndani na nje ya nchi ambao kwa pamoja wamejadili changamoto zinazoikabili sekta ya utalii na ukarimu na kushirikishana uzoefu katika kupata suluhisho.
“Kongamano hili liwe mwanzo mzuri wa kuendelea na mijadala mingine kwa siku zijazo kwa lengo la kupata mawazo yatayosaidia kukuza sekta ya utalii”,alisema Meja Jenerali Gaugence Milanzi.
Alisema serikali kwa upande wake itaendelea kuimarisha ulinzi na usalama kwa kuwa ni kivutio kimojawapo kwa wageni na watalii hivyo kuwataka wananchi kuunga mkono juhudi hizo kwa kuendelea kuwa wakarimu kwa watalii na wageni.
Aidha aliwaasa wananchi kutokuwa na mawazo hasi kwa sheria ya ongezeko la kodi (VAT) katikalinaloigusa sekta ya utalii na ukarimu kwani ina malengo mazuri ya kuongeza mapato ya serikali ambayo yatatumika katika uboreshaji wa huduma za jamii na miundombinu.
“Tujipe muda wa kuona matokeo ya utekelezaji wa sheria hii badala ya kuwa na mawazo hasi kwa sheria hiyo”
Kwa upande wao, waandaji na washiriki wa kongamano hilo wameishauri serikali kuwatumia wataalamu na watafiti hapa nchini katika sekta ya utalii na ukarumu ili mchango wao usaidie kuboresha sekta hiyo katika kukuza uchumi wa nchi.
Akiwasilisha majumisho ya kongamano hilo, Daktari Shogo Mlozi, Mhadhiri na Mkuu Idara ya Utalii na Ukarimu ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania alisema kuwa serikali iwatumie wataalamu na watafiti kutoka hapa nchini katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto katika sekta ya utalii na ukarimu.
“Ni muhimu serikali ikahusisha wataalamu katika uundaji wa sera na miongozo mbalimbali kwani watatoa utalaamu wao kwa manufaa ya Taifa”, alisema Dkt. Mlozi.
Alisema kuwa watafiti na wanataluuma wana nafasi kubwa ya kutoa mchango katika uboreshaji sekta ya utalii kupitia tafiti ambazo zikizingatiwa zinaweza kusaidia katika uboreshaji wa sekta ya utalii hivyo kuiimarisha sekta hii muhimu kwa uchumi wa taifa.
Kwa upande wake Mkuu wa Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Jamii, Dkt.Felician Mutasa alisema kuwa kuna hazina kubwa ya wataalamu ambao wakishirikishwa wanaweza kutoa mchango katika sekta ya utalii kupitia tafiti, ushauri na uboreshaji wa sera ya utalii kwa manufaa ya nchi.
Profesa Elifas Bisanda, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania alisema kuwa bado kuna changamoto nyingi katika sekta ya utalii lakini zaidi katika ukarimu amabapo watanzania hawajajidhatiti katika utoaji huduma bora kwa watalii na wageni.
Akitolea mfano changamoto wa huduma za hoteli hasa kwa upande wa chakula alisema kuwa si ajabu mgeni anaweza kuambiwa asubiri kwa muda fulani na hatimaye akaambiwa chakula bado hata baada ya muda huo kupita swala linaloitia doa sekta hii ukilinganisha na huduma katika hizohizo katika nchi nyingine.
“Jambo la msingi ni kujitathimini ni kwa namna gani tunawajali wageni na watalii katika utoaji wa huduma”,alisema Profesa Bisanda.
Alisema kuwa kuna umuhimu wa jamii kuelimishwa ili ijue namna ya kuwahudumia na zaidi kuwajali wageni na watalii ili kuwafanya wapende kuja Tanzania na wawe mabalozi wazuri wakirudi nchini kwao.
Kwa miaka ya hivi karibuni takwimu zinaonesha kuwa sekta ya utalii imetoa mchango mkubwa katika pato la taifa wa hadi aslimia zaidi ya 17 na asilimia 25 ya fedha za nje hivyo ni muhuimu serikali ikaipa kipaumbele.
Kongamano hilo la kimataifa katika Utalii na Ukarimu liliandaliwa na Idara ya Utalii na Ukarimu ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikewemo Shirika la Hifadhi la Taifa, Serena Hotels, Leopard Tours Limited, Hyatt Regency na Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha na Kituo cha Mikutano cha Mwlalimu Julius Nyerere.



Tanzanians urged to maintain kindness to attract tourists
By Vincent Mpepo-OUT
Tanzanians have been urged to maintain kindness behaviour to tourists and other foreigners who are coming in the country for tourism activities as a way to boost the country’s economy through the tourism sector.
The statement was made by Minister of Natural Resources and Tourism, Professor Jumanne Maghembe during the official opening of the International Conference on Tourism and Hospitality organized by the Department of Tourism and Hospitality Management of the Open University of Tanzania. 
Minister Maghembe said apart from having good tourism attractions in the country, Tanzanians also need to behave in a good manner so as to attract more tourists who might be good ambassadors to their homelands.
“Tourists expects to meet people who are helpful and supportive in at least giving some explanations or support if needed”, said Prof Maghembe.
He said the government will keep on creating friendly environment in terms of security, protection of the national parks and promoting tourist attractions internationally so as to attract more tourists in the country.
He said in combating poaching the government has continued to strengthen the security in the national parks by employing new security technologies and there is an indication that they have been able to arrest illegal poachers and their network.
“Recently, we have arrested not only small hunters but also the financers and transporters who were not discovered in the past days”, said the Minister Maghembe.
On the collaboration with higher learning institutions, the minister said the government is willing to collaborate with universities in research areas that will contribute to provision of the solutions to the current challenges.
On his side, the Vice Counselor of the Open University, Prof.Elifas Bisanda said the University is implementing one of its responsibilities in sharing the findings of researches to the community through various presentations from academicians.
“Universities have three functions, teaching, research and consultancy and here we are providing services to the society “, said Prof Bisanda.
He also urged academicians and researchers to do more researches on the challenges that are facing the tourism sector thus providing solutions for the betterment of the country.
The Deputy Vice Chancellor responsible for Academics, Professor Deus Ngaruko thanked the Minister for coming and officiating the conference and his assurance to the Open University of Tanzania that his ministry will support the university on the research area.
A two days International Conference on Tourism and Hospitality was organized by the Department of Tourism and Hospitality Management of the Open University of Tanzania with the support from Arusha International Conference Centre, Serena Hotels, Tanzania National Parks, Leopard Tours Limited, Hyatt Regency and Julius Nyerere International Convention Centre.


Serikali Kushirikisha Wataalamu Kuikwamua Sekta ya Utalii, Ukarimu
Na Vincent Mpepo-OUT
Serikali imesema kuwa itaendelea kushirikisha wataalamu na watafiti katika kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazoikabili sekta ya Utalii na Ukarimu ili kuibua fursa na bidhaa mpya kupitia sekta hiyo kwa lengo la kuongeza pato la taifa.
Kauli hiyo imetolewa na Meja Jenerali Gaugence Milanzi, Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii wakati akifunga wa Kongamano la Kimataifa la Utalii, Ukarimu na Ubunifu  kwa Nchi zinazoendelea jijini Dar es salaam lililoandaliwa na Idara ya Utalii na Ukarimu ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
Alisema kuwa kongamano hilo limekuwa mwanzo mzuri wa kuwakutanisha wataalamu, watafiti na wadau wa ndani na nje ya nchi ambao kwa pamoja wamejadili changamoto zinazoikabili sekta ya utalii na ukarimu na kushirikishana uzoefu katika kupata suluhisho.
“Kongamano hili liwe mwanzo mzuri wa kuendelea na mijadala mingine kwa siku zijazo kwa lengo la kupata mawazo yatayosaidia kukuza sekta ya utalii”,alisema Meja Jenerali Gaugence Milanzi.
Alisema serikali kwa upande wake itaendelea kuimarisha ulinzi na usalama kwa kuwa ni kivutio kimojawapo kwa wageni na watalii hivyo kuwataka wananchi kuunga mkono juhudi hizo kwa kuendelea kuwa wakarimu kwa watalii na wageni.
Aidha aliwaasa wananchi kutokuwa na mawazo hasi kwa sheria ya ongezeko la kodi (VAT) katikalinaloigusa sekta ya utalii na ukarimu kwani ina malengo mazuri ya kuongeza mapato ya serikali ambayo yatatumika katika uboreshaji wa huduma za jamii na miundombinu.
“Tujipe muda wa kuona matokeo ya utekelezaji wa sheria hii badala ya kuwa na mawazo hasi kwa sheria hiyo”
Kwa upande wao, waandaji na washiriki wa kongamano hilo wameishauri serikali kuwatumia wataalamu na watafiti hapa nchini katika sekta ya utalii na ukarumu ili mchango wao usaidie kuboresha sekta hiyo katika kukuza uchumi wa nchi.
Akiwasilisha majumisho ya kongamano hilo, Daktari Shogo Mlozi, Mhadhiri na Mkuu Idara ya Utalii na Ukarimu ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania alisema kuwa serikali iwatumie wataalamu na watafiti kutoka hapa nchini katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto katika sekta ya utalii na ukarimu.
“Ni muhimu serikali ikahusisha wataalamu katika uundaji wa sera na miongozo mbalimbali kwani watatoa utalaamu wao kwa manufaa ya Taifa”, alisema Dkt. Mlozi.
Alisema kuwa watafiti na wanataluuma wana nafasi kubwa ya kutoa mchango katika uboreshaji sekta ya utalii kupitia tafiti ambazo zikizingatiwa zinaweza kusaidia katika uboreshaji wa sekta ya utalii hivyo kuiimarisha sekta hii muhimu kwa uchumi wa taifa.
Kwa upande wake Mkuu wa Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Jamii, Dkt.Felician Mutasa alisema kuwa kuna hazina kubwa ya wataalamu ambao wakishirikishwa wanaweza kutoa mchango katika sekta ya utalii kupitia tafiti, ushauri na uboreshaji wa sera ya utalii kwa manufaa ya nchi.
Profesa Elifas Bisanda, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania alisema kuwa bado kuna changamoto nyingi katika sekta ya utalii lakini zaidi katika ukarimu amabapo watanzania hawajajidhatiti katika utoaji huduma bora kwa watalii na wageni.
Akitolea mfano changamoto wa huduma za hoteli hasa kwa upande wa chakula alisema kuwa si ajabu mgeni anaweza kuambiwa asubiri kwa muda fulani na hatimaye akaambiwa chakula bado hata baada ya muda huo kupita swala linaloitia doa sekta hii ukilinganisha na huduma katika hizohizo katika nchi nyingine.
“Jambo la msingi ni kujitathimini ni kwa namna gani tunawajali wageni na watalii katika utoaji wa huduma”,alisema Profesa Bisanda.
Alisema kuwa kuna umuhimu wa jamii kuelimishwa ili ijue namna ya kuwahudumia na zaidi kuwajali wageni na watalii ili kuwafanya wapende kuja Tanzania na wawe mabalozi wazuri wakirudi nchini kwao.
Kwa miaka ya hivi karibuni takwimu zinaonesha kuwa sekta ya utalii imetoa mchango mkubwa katika pato la taifa wa hadi aslimia zaidi ya 17 na asilimia 25 ya fedha za nje hivyo ni muhuimu serikali ikaipa kipaumbele.
Kongamano hilo la kimataifa katika Utalii na Ukarimu liliandaliwa na Idara ya Utalii na Ukarimu ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikewemo Shirika la Hifadhi la Taifa, Serena Hotels, Leopard Tours Limited, Hyatt Regency na Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha na Kituo cha Mikutano cha Mwlalimu Julius Nyerere.