Serikali kuhamasisha
wananchi kuuelewa mpango wa kuondoa ukatili kwa wanawake na watoto
Na Vincent Mpepo-OUT
Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wa ndani na
nje imekusudia kuanza utekelezaji wa mpango kazi wa miaka mitano wenye lengo la
kumaliza kabisa vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto hapa nchini.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu, Wizara ya Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi Sihaba Nkinga wakati wa mafunzo ya siku moja kwa
waandishi wa habari ikiwa ni maandalizi ya uzinduzi wa Mpango Kazi wa Kitaifa
wa kumaliza ukatili kwa wanawake na watoto iliyofanyika jijini Dar es salaam.
Bi alisema kuwa serikali imekusudia kushirikisha waizara na
idara mbalimbali katika utekelezaji wa mpango huo ili kujenga dhana ya upamoja
na kuifikia Jamii kwa haraka hivyo kurahisisha upatikanaji wa taarifa muhimu
kuhusu masuala ya haki za wanawake na watoto.
“Uhamasishaji kwa jamii kuuelewa mpango kazi huu ni jukumu la
kila mmoja wetu hivyo tunapaswa kushirirkiana ili kufanikisha adhma hii ya kuwakomboa
Wanawake na watoto dhidi ya vitendo vya ukatili dhidi yao”, alisema Bi Nkinga
Alisema kuwa serikali imejidhatiti kushirikiana na wadau wa
maendeleo kufanikisha mpango huo ili kulinda hadhi tulipewa kama nchi kwa kuwa
Tanzania ndiyo nchi pekee kwa Afrika amabayo imeonesha utekelezaji kwa vitendo
ijapokuwa juhudi zaidi zinahitajika ili kufikia malengo.
Aidha alisema kuwa uhamasishaji na utekelezaji wa mpango kazi
huo utahusisha asasi za kiraia na taasisi mabalimbali sizizo za kiserikali na
dini.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Watoto, Wizara ya
Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee
na Watoto Bi Maragareth Mussai alisema kuwa mpango kazi huo umezingatia masuala mtambuka ikiwemo
utengaji wa bajeti kwa makundi mbalimbali yanayojishughulisha na Wanawake na
watoto.
“Bajeti imewekwa katika ngazi zote ili kurahisisha
utekelezaji wa mpango kazi huu ikiwemo uwezeshaji kwa wafanyakazi katika idara
mbalimbali katika ununuzi wa vifaa, vyombo vya usafiri na vitendea kazi”,
alisema Bi Mussai.
Naye pedro Guerra, Mtaalamu wa Masuala ya Haki za watoto
alisema kuwa watoto ni waathirika wakubwa wa vitendo vya ukatili hivyo
huathirika kisaikolojia na makuzi ya ubongo wao.
“Matokeo ya tafiti tulizofanya yananoessha watato wa Tanzania
wanakabiliwa na msongo wa mawazo katika ngazi ya familia, mazingira ya shule na
wanaowafanyia ukatili huo ni ndugu wa karibu”, alisema Guerra.
Madhumuni ya mafunzo hayo ya siku moja yalikuwa ni
kuwafundisha waandishi wa habari namna ya kuripoti habari mbalimbalimbali kuhusu
vitendo vya ukatili dhidi ya watoto na Wanawake Tanzania.
No comments:
Post a Comment